Thursday, August 6, 2020

KANUNI ZA KIKUNDI CHA IKICHA


 

 KANUNI ZA IKICHA





S.L.P 44

KIGOMA.


E-MAIL: ikichagroup@gmail.com


TOLEO NA. 2, 2019







YALIYOMO                                                                                                                        UKURASA


SEHEMU YA KWANZA: UTANGULIZI

KAULI MBIU……………….…………………………………………………….………….……….3

NEMBO YA KIKUNDI……….…………………………………...………………...….................….3

ANUANI…………………………..…………………………………..…………….…..……………3

SEHEMU YA PILI: UANACHAMA

SIFA ZA MWANACHAMA………………………………………………………………………...3

HAKI ZA MWANACHAMA……………………………………………….………………………3

WAJIBU WA MWANACHAMA……………………………………………………………………4

SEHEMU YA TATU: UONGOZI WA KIKUNDI

UONGOZI WA KIKUNDI………………………..…………………………………................…..4

UCHAGUZI WA VIONGOZI…………………………………………………………...................4

SEHEMU YA NNE: MIKUTANO NA VIKAO VYA KIKUNDI

MIKUTANO NA VIKAO VYA KIKUNDI………………………………………………………..5

UDHURU…………………………………………………………………….…………..……….5

MSIBA………..…………………………………………………………………………………5

MAGONJWA…………………………………………………………………………………....5

KIKAZI…………………………………………………………….……………………………5

SAFARI YA LIKIZO………………………………………………………….............................5

SEHEMU YA TANO: MAPATO YA KIKUNDI

VYANZO VYA MAPATO YA KIKUNDI…..………..……………………………….…….…6

ADA YA KIINGILIO…………………………………………………………………………6

ADA YA MWEZI………………………………………………………………………………6

MICHANGO MINGINE…………………………………………………….....………………..7

MISIBA…………………………………………………………………………………………7

HARUSI…………………………………………………………………………………………7

MAGONJWA……………………………………………………..……………………………..8

ANAYEHAMA NJE YA MANISPAA…………………………………………………………8

MIKOPO………………………………………………………………………………………..8

MADENI YA KIKUNDI………………………………………………………………………10

SEHEMU YA SITA: UTUNZAJI WA MALI NA FEDHA ZA KIKUNDI

UTUNZAJI WA FEDHA ZA KIKUNDI…………………………………..……......…………..10

KIKOKOTOO CHA HISA…………………………………………………………………………10

SEHEMU YA SABA: KUVUNJIKA KWA KIKUNDI

KUVUNJIKA KWA KIKUNDI……………………………………………………………………11












SEHEMU YA KWANZA


1. 0 UTANGULIZI

1. 1 KAULI MBIU

1. 1.1 Kauli mbiu itatumika kwenye vikao,mikutano na matukio mbalimbali ya

kikundi kama salamu rasmi.

1.1.2 Kauli mbiu itatumika kwenye nyaraka zote zinazohusiana na kikundi.

I.2 NEMBO YA KIKUNDI

I.2.1 Nembo itatumika kwenye nyaraka zote zinazohusiana na kikundi.

I.2.2 Nembo itatumika kwenye sare zote za kikundi.

I.3 ANUANI

I.3.1 Itatumika kwenye barua zote za kikundi.


SEHEMU YA PILI


2.0 UANACHAMA

2.1 SIFA ZA MWANACHAMA

2. 1.1 Mtu yeyote anayeomba kujiunga na kikundi atapaswa kuwa na mdhamini

ndani ya kikundi atakayemsainia kwenye fomu ya kujiunga.

2.1.2 Mtu yeyote anayeomba kujiunga na kikundi atajadiliwa kwanza na

wanakikundi kabla ya kusajiliwa.

2.1.3 Kiambatisho kwenye fomu ya kujiunga na kikundi kitakuwa ni kivuli cha

Kitambulisho cha Taifa(NIDA)/Hati ya Kusafiria , kama nyaraka hizo hazipo

kiambatisho kitakuwa kitambulisho cha mpiga kura ama Leseni ya udereva.

2.1.4 Kila mwanachama atatakiwa kujaza fomu ya kujiunga na kikundi.

2.2 HAKI ZA MWANAKIKUNDI

2.2.1 Mwanakikundi akitaka kujitoa anatakiwa kutoa taarifa mwezi mmoja kabla kwa

maandishi ili aandaliwe stahiki zake.

2.2.2 Mwanakikundi anapaswa kulipa madeni yake yote anayodaiwa na kikundi

kabla ya kujitoa,kama atashindwa kulipa atakatwa kwenye Hisa/Stahiki

zake.


2.2.3 Uhuru wa kutoa maoni uwe na mipaka na maoni yaendane na dhima ya


kikundi.


2.2.4 Mwanakikundi atakuwa na uhuru wa kukopa fedha wakati wowote ikiwa


atatimiza vigezo na masharti ya ukopaji.


2.2.5 Mwanakikundi atabaki na uanachama wake ndani ya kikundi hata

akihama nje ya manispaa kwa kuzingatia sharti la kutokopa zaidi ya hisa

zake.


2.3 WAJIBU WA MWANAKIKUNDI


2.3.1 Kutoshiriki kwenye shughuli za kikundi kama vile magonjwa, misiba,

harusi, miradi n.k, faini yake itakuwa Tsh.5000/=kwa kila shughuli/tukio

ambalo mtu hakushiriki.


2.3.2 Mwanakikundi atakayekiuka maagizo rasmi ya kikundi atatozwa faini ya


Tsh. 5000/=.


2.3.3 Mwanachama atapewa maagizo rasmi ya kikundi mara mbili tu na

asipotekeleza kwa wakati aliopewa atatozwa faini ya Tsh.5000/=.

2.3.4 Mwanakikundi atatakiwa kutoa rambirambi kutokana na Vifo

vinavyotambuliwa na kikundi ambavyo ni mwanakikundi

kufariki,baba,mama,mme,mke au mtoto.


2.3.5 Vikao vya kikundi vitafanyika kila Jumapili ya kwanza ya kila mwezi.

2.3.6 Mwanakikundi ambaye hatatoa ushirirkiano wa kutosha /ipasavyo atapewa


adhabu mojawapo kati ya hizi zifuatazo;


a/ Onyo la mdomo.

b/ Faini ya Tsh.5,000/=.

2.3.7 Kikundi kitakuwa kinagharimia nauli zitakazokuwa zinatumika katika


shughuli za kikundi.


SEHEMU YA TATU


3.0 UONGOZI WA KIKUNDI

3.1 Kiongozi atakayeshindwa kutekeleza majukumu yake atapewa adhabu

mojawapo kati ya hizi kulingana na kosa alilofanya, adhabu hizo ni;

a. Onyo la mdomo ama la maandishi.

b. Kulipa faini ya Tsh.10,000/=.

c. Fidia

d. Kusimamishwa uongozi kwa muda wa siku tisini (90).

e. Kuondolewa kwenye Uongozi.

3.2 Iwapo kiongozi atajiuzuru, atajitoa ama kutolewa kwenye kikundi ama

akihama uchaguzi wa nafasi yake utafanyika ndani ya mwezi mmoja.

3.3 Iwapo kiongozi atakuwa katika hali ya kuugua kwa muda wa miezi sita (06)

mfululizo nafasi yake itakaimiwa na mwanakikundi atakayependekezwa na

wanakikundi.

3.4 Iwapo kiongozi atafungwa jela nafasi yake itakaimiwa na mwanakikundi

atakayekuwa amependekezwa na wanakikundi hadi uchaguzi utakapofanyika.


3.5 UCHAGUZI WA VIONGOZI

I. Kwa nafasi ya Mwenyekiti na Katibu, yatapendekezwa majina matatu (3)

na kuyapigia kura za siri na mshindi wa kwanza ndiye atakayekuwa

MKUU na anayefuata kwa kura atakuwa MSAIDIZI wake.

II. Kwa nafasi ya Mhasibu, yatapendekezwa majina mawili na kuyapigia kura

za siri atakayepata kura nyingi ndiye atakayekuwa Mhasibu wa kikundi.


SEHEMU YA NNE

4.0 MIKUTANO NA VIKAO VYA KIKUNDI

4.1 UDHURU

a) MSIBA

i. Ruhusa za msiba zitatolewa iwapo mwanakikundi amefiwa na baba,

mama, mke, mume au mtoto.

b) MAGONJWA

i. Ruhusa za magonjwa zitatolewa iwapo mwanakikundi mwenyewe

amelazwa siku ya kikao.


c) KIKAZI

d) SAFARI YA LIKIZO

4.2 Mwanakikundi anawajibika kuwahi vikao na mikutano ya kikundi.

4.3 Mwanakikundi atatakiwa kutoa taarifa ya kuchelewa ama kutofika kwenye

vikao/mikutano ya kikundi saa moja kabla ya kikao/mkutano kuanza.

4.4 Iwapo mwanakikundi atachelewa kutoa taarifa ya kuchelewa kufika kwenye

kikao/mkutano atatozwa faini ya Tsh.1000/=.

4.5 Iwapo mwanakikundi hatatoa taarifa ya kuchelewa kufika kwenye

kikao/mkutano na akachelewa kufika kwenye kikao/mkutano atatozwa faini

ya Tsh.2000/=.

4.6 Iwapo mwanakikundi atachelewa kutoa taarifa ya kutohudhuria kwenye

kikao/mkutano atatozwa faini ya Tsh.3000/=.

4.7 Iwapo mwanakikundi hatatoa taarifa ya kutohudhuria kwenye kikao/mkutano

atatozwa faini ya Tsh.5000/=.

4.8 Iwapo mwanakikundi hatahudhuria kikao/mkutano kwa sababu zisizokubalika

katika Kanuni za Kikundi atatozwa faini ya Tsh.5000/=.

4.9 Iwapo mwanakikundi hatohudhuria kwenye kikao/mkutano atatozwa faini ya

Tsh.5000/=.

4.10 Hata kama kikao/mkutano utaahirishwa kwa sababu ya Akidi kutotimia, faini

iliyotajwa kwenye kifungu cha 4.3,4.4,4.5,4.6,4.7 na 4.8 itabaki pale pale.

4.11 Taarifa zote za kuchelewa ama kutohudhuria kikao/mkutano zitolewe kwa

Mwenyekiti/Katibu wa kikundi kwa njia ya meseji za simu/barua/kufika

mwenyewe kwenye kikao/mkutano.


SEHEMU YA TANO


5.0 MAPATO YA KIKUNDI

5.1 VYANZO VYA MAPATO YA KIKUNDI

5.1.1 ADA YA KIINGILIO

I. Mwanakikundi atasajiliwa kwenye kikundi baada ya kulipa kiingilio cha

Tsh. 50,000/=.

II. Kiingilio kitalipwa mara moja tu wakati wa kujiunga.


5.1.2 ADA YA MWEZI

I. Ada itakuwa inalipwa kila mwezi.

II. Ada ya mwezi ni Tsh. 12,000/=.

III. Kipindi cha Neema (Grace Period) cha kulipa ada kitaanza tarehe 01 hadi

tarehe 07 ya kila mwezi.

IV. Mwanakikundi atakayechelewa kulipa ada ya kila mwezi atapewa kipindi

cha Neema cha siku saba baada ya hapo kama atakuwa hajalipa

atatozwa faini ya Tsh.2000/= ambayo itakuwa ikiongezeka kwa kiasi

hicho hicho kila baada ya siku saba hadi hapo ada itakapokuwa

imetolewa.

V. Risiti itawasilishwa kwenye kikao cha kila mwezi.

VI. Mwanakikundi asipotoa Ada ya kila mwezi kwa muda wa miezi mitatu (03)

mfululizo bila taarifa rasmi kwa uongozi atakuwa amejifuta uanachama wa

kikundi.

VII. Mwanakikundi atakayelipa ada kwa njia ya simu atalipa makato ya benki.

VIII. Mwanakikundi atahesabika amelipa ada baada ya kuwasilisha risiti ya

malipo.

IX. Mwanakikundi anatakiwa kulipa faini ndani ya miezi mitatu, na ikiingia

mwezi wa nne na kuendelea faini itaongezeka kwa asilimia mia(100%)

kwa kila mwezi.


5.1.3 MICHANGO MINGINE YA KIKUNDI

I. MISIBA

a) Kila mwanakikundi anatakiwa kutoa mchango wa Tsh.5000/= kwa ajili ya

pole kwa mfiwa.

b) Mchango huu utatolewa iwapo mwanachama ataondokewa na baba,

mama, mme, mke au mtoto.

c) Iwapo mwanakikundi amefariki kila mwanachama atatakiwa kutoa

mchango wa Tsh.10,000/=.

d) Mwanakikundi akifariki stahili zake zote atapewa mrithi aliyeainishwa

kwenye fomu ya kujiunga na uanachama.

e) Mwanakikundi ambaye hatakuwa ametoa mchango huu atakatwa

Tsh.5000/= au 10,000/= kutoka kwenye Ada yake ya kila mwezi.

f) Kiasi hicho kilichokatwa kwenye ada yake ya kila mwezi kitatakiwa

kirudishwe ndani ya mwezi mmoja tangu kilipokatwa.

g) Mchango wa rambirambi utatolewa ndani ya siku saba (7) tangu taarifa

ilipotolewa.

h) Mrithi atapewa stahili zake ndani ya siku 14 tangu ilipotolewa taarifa ya

msiba.


II. HARUSI

a) Mchango wa harusi utamhusu mwanakikundi tu.

b) Kila mwanakikundi atatoa Tsh.5000/= ambao utakuwa mchango kwa ajili

ya zawadi .

c) Mwanakikundi ambaye hatakuwa ametoa mchango huu atakatwa

Tsh.5000/= kutoka kwenye Ada yake ya kila mwezi.

d) Kiasi hicho kilichokatwa kwenye ada yake ya kila mwezi kitatakiwa

kirudishwe ndani ya mwezi mmoja tangu kilipokatwa.

e) Taarifa itolewe mwezi mmoja kabla ya harusi.


III. MAGONJWA

a) Kila mwanakikundi atatoa Tsh.5000/= kwa ajili ya mgonjwa.

b) Mwanakikundi ambaye hatakuwa ametoa mchango huu atakatwa Tsh.5000/=

kutoka kwenye Ada yake ya kila mwezi.

c) Kiasi hicho kilichokatwa kwenye ada yake ya kila mwezi kitatakiwa kirudishwe

ndani ya mwezi mmoja tangu kilipokatwa.

d) Mchango utatolewa kwa mwanachama ambaye amelazwa kuanzia siku tatu au

yuko kwenye hali mbaya sana.

e) Mwanakikundi atakayeumwa atapaswa kuleta vielelezo vya matibabu yake ili

achangiwe.

IV. ANAYEHAMA NJE YA MANISPAA

a. Kila mwanakikundi atatoa Tsh.5000/= kwa ajili ya zawadi ya kumuaga

Mwanakikundi anayehama.

b. Mwanakikundi ambaye hatakuwa ametoa mchango huu atakatwa

Tsh.5000/= kutoka kwenye Ada yake ya kila mwezi.

c. Kiasi hicho kilichokatwa kwenye ada yake ya kila mwezi kitatakiwa

kirudishwe ndani ya mwezi mmoja tangu kilipokatwa.

5.2 MIKOPO

5.2.1 Mwanakikundi anayeomba mkopo anatakiwa ajaze fomu ya maombi ya

mkopo.

5.2.2 Mwanakikundi anayetaka kukopa atatakiwa awe na mdhamini mmoja

ndani ya kikundi.

5.2.3 Mwanakikundi atapewa mkopo baada ya kutimiza masharti yote na iwapo

fedha ipo.

5.2.4 Utoaji wa mkopo utazingatia ombi lililotangulia.

5.2.5 Mwanakikundi atatakiwa kurejesha mkopo kwanza kabla ya kukopa tena.

5.2.6 Mwanakikundi mwenye deni lolote la ada,rejesho,faini ama michango

mingine hataruhusiwa kuchukua mkopo.

5.2.7 Mwanakikundi mpya ataruhusiwa kukopa baada ya miezi mitatu tangu

alipojiunga.

5.2.8 Mwanakikundi asiye na ajira ya kudumu ataruhusiwa kukopa kiasi

kinacholingana na hisa yake na kujumlisha kiasi cha nusu ya hisa yake.

5.2.9 Mwanakikundi atakayechukua mkopo atatakiwa kurejesha riba ya 10% ya

mkopo aliochukua.

5.2.10 Iwapo mwanakikundi atafariki akiwa na deni la kikundi na hisa zake ni

ndogo kuliko deni, atasamehewa deni hilo ila hisa zake zitabaki kuwa mali

ya kikundi.

5.2.11 Iwapo mwanakikundi atafariki akiwa na deni la kikundi na hisa zake ni

kubwa kuliko deni, hisa zake zitalipa deni hilo na kitakachobaki atapewa

mrithi wake.

5.2.12 Mwanakikundi atatakiwa kurejesha mkopo kama ifuatavyo;

I. 0000 - 100,000/=Marejesho ya Mkopo na Riba yafanyike ndani ya

mwezi mmoja (01).

II. 100,001-500,000/=Marejesho ya Mkopo na Riba yafanyike ndani ya

miezi mitatu (03).

III. 500,001- 1000,000/= Marejesho ya Mkopo na Riba yafanyike kila

mwezi ndani ya miezi sita (06) kwa uwiano wa moja ya sita (1/6).

IV. 1000,001- 1200,000/= Marejesho ya Mkopo na Riba yafanyike kila

mwezi ndani ya miezi saba (07) kwa uwiano wa moja ya saba(1/7).

V. 1200,001-1500,000/= Marejesho ya Mkopo na Riba yafanyike kila

mwezi ndani ya miezi nane (08) kwa uwiano wa moja ya nane(1/8).

5.2.13 Kama mwanakikundi atachelewa kurejesha rejesho lake la kila mwezi

atapewa kipindi cha Neema cha siku saba ,akiingia siku ya nane na

kuendelea rejesho lake litapigiwa 10% kama faini.

5.2.14 Iwapo mwanakikundi ameshindwa kurejesha mkopo wake kwa wakati na

kwa masharti aliyopewa sheria za kikundi na za nchi zitafuatwa

5.2.15 Mtu yeyote asiyekuwa mwanachama hataruhusiwa kupewa mkopo.

5.2.16 Mhasibu atatakiwa kuitaarifu Kamati ya Fedha na Mikopo kabla ya

kupitisha fomu ya mkopo wa mwanakikundi.

5.2.17 Watia saini watapewa nauli na kikundi watakapokuwa wanashughulikia

masuala ya fedha benki.


5.3 MADENI YA KIKUNDI.


I. Kila mwanakikundi anahusika kikamilifu na madeni ya kikundi kama

deni hilo halikusababishwa na uzembe wa mwanakikundi.

II. Deni binafsi la mwanakikundi si deni la kikundi na kikundi hakitahusika

kwa vyovyote vile.

III. Mkopo utakaohusu kikundi, wanakikundi wote washirikishwe katika

hatua zote na muhtasari uwepo wa kuthibitisha maazimio ya uchukuaji

wa mkopo huo.



SEHEMU YA SITA


6.0 UTUNZAJI WA MALI NA FEDHA ZA KIKUNDI

6.1 UTUNZAJI WA FEDHA ZA KIKUNDI.

I. Kila mwanakikundi ataweka Ada, Marejesho na Faini yake kwenye

Akaunti ya kikundi.

II. Mabadiliko yoyote ya Akaunti ya Benki ya kikundi yatatakiwa

kuwasilishwa, kujadiliwa na kupitishwa katika vikao vya kikundi.

III. Mhasibu na Kamati ya Fedha na Mikopo wataandaa Taarifa ya Fedha

ya Nusu mwaka na ya mwaka na kuiwasilisha kwa kamati Tendaji ya

kikundi.


6.2 KIKOKOTOO CHA HISA, kitakuwa;

JUMLA YA ADA ALIZOLIPA MWANACHAMA TANGU ALIPOJIUNGA NA

KIKUNDI JUMLISHA JUMLA YA FAIDA ILIYOPATIKANA KILA MWEZI KWA

MIEZI YOTE TANGU ALIPOJIUNGA NA KIKUNDI HADI TAREHE YA KUJITOA

/KUTOLEWA KWENYE KIKUNDI GAWANYA KWA IDADI YA WANACHAMA

KWA KILA MWEZI.

SAWA NA;


JUMLA YA ADA + JUMLAYA FAIDA YA KILA MWEZI KWA MIEZI YOTE


IDADI YA WANACHAMA KILA MWEZI


SEHEMU YA SABA


7 .0 KUVUNJIKA KWA KIKUNDI

I. Kikundi kitavunjika iwapo robo tatu ya wanakikundi wameridhia kuvujika.

II. Endapo kikundi kitabaki na wanakikundi wawili, kitatakiwa kivunjwe.

III. Kikundi kikivujwa/kuvunjika wanakikundi ambao watakuwa hai ndio watakao

gawana mali zote za kikundi.

IV. Maamuzi ya kuvunja kikundi yatafanyika katika kikao halali cha kikundi na

muhtasari utaandikwa.

V. Kabla ya kuvunja kikundi, pesa zote za kikundi zitatakiwa kuwekwa kwenye

Akaunti ya kikundi.

VI. Kabla ya kuvunja kikundi, madeni yote ya kikundi yanatakiwa kulipwa kwanza.

VII. Kabla ya kuvunja kikundi, mali zote za kikundi zitatakiwa kuwasilishwa

kwenye kikao cha kuvunja kikundi.


IKICHA…,


TUINUANE KATIKA MAENDELEO

No comments:

Post a Comment