Thursday, August 6, 2020

MKUTANO MKUU 2019

 Kikundi cha IKICHA huwa kina utamaduni wa kufanya mkutano mkuu na wanakikundi katika kila mwisho wa mwaka. Mkutanao huwa unapangwa na kikao cha mwezi wa 12 na shughuli za mkutano mkuu ni kujadili taarifa za kamati mbalimbali kama vile fedha na mikopo, uchumi na mipango, maafa na sherehe, katiba na sheria.

Taarifa hizi huwasilishwa na wenyeviti wa kamati hizo na kujadiliwa na wanakikundi. Lakini pia wajumbe wa mkutano mkuu wa mwaka huwa wanafanya uchaguzi kwa viongozi wa chama na makabidhiano huwa yanafanyika kwa viongozi wapya waliochaguliwa.

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama wakifuatilia taarifa zilizokuwa zinawasilishwa.
Mkutano Mkuu ukiendelea huku wajumbe wakiendelea kupata viburudisho.
Mwenyekiti na Katibu Mkuu waliomaliza muda wao katika uongozi wakiwa wanaendesha mkutano mkuu.
Mwenyekiti aliyechaguliwa kwenye Mkutano Mkuu  Alex Kamalinge akitoa neno la shukrani baada ya kuchaguliwa na wajumbe wa Mkutano Mkuu na aliyekaa hapo ni Katibu Mkuu wake Scola Wilson.
Baada ya uchaguzi makabidhiano huwa yanafanyika na hapo katika picha ni Ndg. Filbert Lukondo (kushoto) akiwa anamkabidhi majalada kwa mwenyekiti mpya wa kamati ya katiba na sheria Ndg. Emmanuel Msabaha.
Katibu Mkuu aliyechaguliwa Bi. Scola Wilson (kulia) akibadhiwa begi la mafaili na aliyekuwa Katibu Mkuu Ndg. Makoko Obadia.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wakifuatilia jambo.

Picha ya pamoja ya wanakikundi wa  IKICHA 

No comments:

Post a Comment