Thursday, August 6, 2020

KATIBA YA KIKUNDI CHA INUA KIPATO CHAKO (IKICHA)

(IKICHA)







S.L.P 44
KIGOMA.

E-MAIL: ikichagroup@gmail.com

KATIBA
TOLEO NA. 2, 2019















YALIYOMO                                                                UKURASA

SEHEMU YA KWANZA: UTANGULIZI
Jina la Kikundi………………………………………………………………………………………….4
Kauli Mbiu ya Kikundi………………………………………………………………………………….4
Nembo ya Kikundi…………………………………………...………………………………………….4
Anuani ya Kikundi……………………………………………………...……………………………….4

SEHEMU YA PILI: MALENGO YA KIKUNDI
Misingi ya Kikundi (Group Core Values)……………………………………………………………….5
Lengo Kuu la Kikundi…………………………………………………………………………………..5
Malengo Mahususi ya Kikundi………………………………………………………………………….5

SEHEMU YA TATU: IDADI YA WANACHAMA,JINSIA NA LUGHA
Idadi ya Wanachama……………………………………………………………………………………5
Jinsia…………………………………………………………………………………………………….5
Lugha……………………………………………………………………………………………………5

SEHEMU YA NNE: UANACHAMA
Kujiunga na Kikundi…………………………………………………………………………………….6
Sifa za Mwanachama…………………………………………………………………..………………..6
Haki za Mwanachama…………………………………………………………………….…………….6
Wajibu wa Mwanachama………………………………………………………………...…………..…6
Ukomo wa Mwanachama……………………………………………………………...……………..…6

SEHEMU YA TANO: UONGOZI WA KIKUNDI
Muundo wa Uongozi……………………………………………………………………………………7
Majukumu ya Viongozi……………………………………..…………………………………………..8
Mwenyekiti…………………………………………………...…………………………………………8
Majukumu ya Mwenyekiti ………….…………………………………………………………….......8
Mwenyekiti Msaidizi…………………………………………………………………………………….8
Majukumu ya Mwenyekiti Msaidizi………………………………………………………………….......8
Katibu…………………………………………………………………………………………………….8
Majukumu ya Katibu…………………………………………………………………………………....8
Katibu Msaidizi…………………………………………………………………………………………..8
Majukumu ya Katibu Msaidizi…………………………………………………………………………...8
Mhasibu………………………………………………………………………………………………....8
Majukumu ya Mhasibu………………………………………………………………………………..9
Kamati za Kikundi……………………………………………………………………………………...9
Kamati ya Katiba na Sheria………………………………………………………………………..….9
Wajumbe wa Kamati ya Katiba na Sheria……………………………………………………………....9
Majukumu ya Kamati……………………………………………………………………………………9
Kamati ya Fedha na Mikopo………………………………………………………………………….….9
Wajumbe wa Kamati ya Fedha na Mikopo……………………………………………………………..9
Majukumu ya Kamati………………………………………………………..……………………….…9
Kamati ya Maafa na Sherehe………………………………………………………………………….….9
Wajumbe wa Kamati ya Maafa na Sherehe…………………………………………………………..…..9
Majukumu ya Kamati……………………………………………………………………………….…10
Kamati ya Uchumi na Mipango……………………………………………………………………….10

KATIBA YA IKICHA
Wajumbe wa Kamati ya Uchumi na Mipango…………………………………………………….......10
Majukumu ya Kamati………………………………………………………………………………....10
Muda wa Uongozi………………………………………………………………………………………10

SEHEMU YA SITA: MIKUTANO NA VIKAO VYA KIKUNDI
Mkutano Mkuu………………………………………………………………………………………..10
Majukumu ya Mkutano Mkuu………………………………………………………………………...10
Vikao vya Kikundi………………………………………………………………………………………11
Majukumu ya Vikao…………………………………………………………………………………...11
Vikao vya dharura………………………………………………………………………………………11
Kamati Tendaji…………………………………………………………………………………………..11
Vikao vya Kamati Tendaji………………………………………………………………………………11
Majukumu ya Kamati Tendaji…………………………………………………………………………11

SEHEMU YA SABA: MAPATO YA KIKUNDI
Vyanzo vya Mapato ya Kikundi……………………………………………………………………….12
Ada ya Kiingilio……………………………………………………………………………………….12
Ada ya kila mwezi……………………………………………………………………………………12
Faida kutokana na Miradi…………………………………………………………………………...12
Riba ya Mikopo……………………………………………………………………………………….12
Miradi mbalimbali…………………………………………………………………………………...12
Faini mbalimbali………………………………………………................…………………………...12
Michango Mingine …………………………………………….............................................………..12
Harusi……………………………………………………………………………………………….12
Magonjwa.………………………………………………………… ……………………………..12
Misiba……………………………………………………………………………..………………….12
Anayehama Nje ya Manispaa…………………………………………………………………………12
Mikopo…………………………………………………………………………………………..……12
Madeni ya Kikundi………………………………………………..……………………………………12

SEHEMU YA NANE: UTUNZAJI WA MALI NA FEDHA ZA KIKUNDI
Utunzaji wa Mali na Fedha za Kikundi……………………………………………………………….13
Upotevu na Uharibifu wa Mali ya Kikundi…………………………………………………..………13

SEHEMU YA TISA: MAREKEBISHO YA KATIBA NA KUVUNJIKA KWA KIKUNDI
Marekebisho ya Katiba ya Kikundi…………………………………………………………….……….13
Kuvunjika Kwa Kikundi……………………………………………………………………………….13

SEHEMU YA KUMI: ORODHA YA WANACHAMA NA SAHIHI ZAO
Orodha ya Wanachama na Sahihi za Wanachama…………………………………………….……..14












SEHEMU YA KWANZA

1.0 UTANGULIZI


1. 1 JINA LA KIKUNDI

IKICHA (INUA KIPATO CHAKO) ni umoja wa baadhi ya Watu wanaoishi
katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji waliokubaliana kuanzisha kikundi kwa malengo
mbalimbali na lengo kuu likiwa Kuwezesha mwanakikundi kujikwamua kiuchumi kwa njia
ya kuweka na kukopa.Kikundi hiki kilianzishwa rasmi tarehe 13/12/2015 kikiwa na
idadi ya wanachama kumi na moja (11).
Katiba hii itajulikana kama Katiba ya kikundi cha IKICHA ya mwaka 2019 ambayo
imetokana na mabadiliko ya katiba, Toleo Na.1,2015 na itakuwa ndio muongozo wa
kuendesha shughuli zote za kikundi.

1.2 KAULI MBIU YA KIKUNDI

1.2.1 Kauli mbiu ya kikundi ni “TUINUANE KATIKA MAENDELEO”

1.3 NEMBO YA KIKUNDI

1.3.1 .Kikundi kitakuwa na NEMBO
1.3.2 NEMBO ya kikundi itakuwa na alama zifuatazo:-
I. Ramani ya Afrika
II. Pesa
III. Nyumba
IV. Gari
V. Mti
VI. Ngazi
VII. Mtu akipanda ngazi


1.4. ANUANI
KIKUNDI CHA INUA KIPATO CHAKO (IKICHA),
MTAA WA LAKE TANGANYIKA.
S.L.P 44,
KIGOMA.
E-mail: ikichagroup@gmail.com


1.5 MISINGI YA KIKUNDI (GROUP CORE VALUES)

I. Upendo
II. Uadilifu
III. Uaminifu
IV. Ukweli na Uwazi
V. Kuheshimiana
VI. Uwajibikaji

KATIBA YA IKICHA

VII. Umoja na Ushirikiano
VIII. Usiri
IX. Bidii
X. Maendeleo

SEHEMU YA PILI

2.0 MALENGO YA KIKUNDI

2.1 LENGO KUU LA KIKUNDI
2.1.1 Kuwezesha mwanakikundi kujikwamua kiuchumi.

2.2 MALENGO MAHUSUSI YA KIKUNDI
I. Kuweka na Kukopa.
II. Kusaidiana katika Shida na Raha.
III. Kuelimishana katika masuala ya Kiuchumi.
IV. Kuanzisha Miradi mbalimbali ya Kiuchumi.

SEHEMU YA TATU

3.0 IDADI YA WANACHAMA,JINSIA NA LUGHA

3.1. IDADI YA WANACHAMA
3.1.1 Kikundi kitakuwa na wanachama 30 tu.
3.2. JINSIA.
3.2.1 Kikundi kitakuwa cha Jinsia zote.
3.3 LUGHA
3.3.1 Lugha ya mawasiliano itakuwa Kiswahili.

SEHEMU YA NNE

4.0 UANACHAMA

4.1 KUJIUNGA NA KIKUNDI
4.1.1 Ni muda wowote kama kuna nafasi.

IV.2 SIFA ZA MWANACHAMA.
I.Awe na umri wa kuanzia miaka 18 na kuendelea.
II.Awe ameajiriwa au kujiajiri.
III.Awe mwaminifu na mwenye tabia njema.
IV.Awe mkazi katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji.
V.Awe mtiifu kwa katiba,sheria na kanuni za kikundi.


4.3 HAKI ZA MWANACHAMA
I.Ana haki ya kuchagua na kuchaguliwa katika uongozi wa kikundi.
II.Ana uhuru wa kutoa maoni.
III. Ana haki ya kujitoa uanakikundi.
IV.Ana haki ya kusaidiwa katika shida na raha.
V.Ana haki ya kujua mapato na Matumizi ya kikundi.
VI.Ana haki ya kujua michango yake.
VII.Ana haki ya kukopa fedha kwenye kikundi.

4.4 WAJIBU WA MWANACHAMA
I.Kuhudhuria vikao/mikutano ya kikundi.
II.Kuchangia michango ya kikundi.
III.Kushiriki shughuli zote za kikundi
IV.Kutunza siri za kikundi.
V.Kulipa mali ya kikundi akiharibu au kupoteza kwa uzembe au makusudi.
VI.Kuwapenda na kuwajali wanakikundi wenzake.
VII.Kulinda na kutunza mali za kikundi.
VIII. Kutoa ushauri kuhusu maendeleo ya kikundi.
IX. Kutekeleza maagizo rasmi ya Kikundi.

4.5 UKOMO WA MWANACHAMA
I. Kifo
II.Kujitoa kwa hiari.
III.Kuvunjika kwa kikundi.
IV.Kufutwa/kusimamishwa na kikundi.
V.Kutohudhuria vikao vitatu mfululizo bila taarifa rasmi na kushindwa kulipa faini yake.
VI.Kutohudhuria kwenye matukio matatu mfululizo ya kikundi bila taarifa na kushidwa
kulipa faini ya kosa hilo.

SEHEMU YA TANO

5.0 UONGOZI WA KIKUNDI

5.1 MUUNDO WA UONGOZI

MWENYEKITI

KATIBA YA IKICHA

MWENYEKITI MSAIDIZI

KATIBU

KATIBU MSAIDIZI

MHASIBU

KAMATI ZA KIKUNDI

WAJUMBE

5.2 MAJUKUMU YA VIONGOZI
5.2.1 MWENYEKITI
5.2.1.1 MAJUKUMU YA MWENYEKITI
I.Kuongoza vikao/ mikutano yote ya kikundi.
II.Kuwa msemaji mkuu wa kikundi.
III.Kusimamia katiba, sheria na kanuni za kikundi.
IV.Kukagua mapato na matumizi ya kikundi.
V. Kusimamia mali za kikundi.
VI. Kugawa kazi kwa wanakikundi.
VII. Kutunza mali za kikundi anazotumia kama mwenyekiti.

5.2.2 MWENYEKITI MSAIDIZI
5.2.2.1 Ni Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba na Sheria.
5.2.2.2 MAJUKUMU YA MWENYEKITI MSAIDIZI
I.Atatekeleza majukumu ya Mwenyekiti wakati Mwenyekiti anapokuwa hayupo kwa
udhuru wowote ule.
II.Kumsaidia Mwenyekiti.


5.2.3 KATIBU

5.2.3.1 MAJUKUMU YA KATIBU
I.Mtendaji mkuu wa kikundi.
II.Kuitisha vikao vya kikundi.
III.Kuandika mihtasari ya vikao na mikutano ya kikundi.
IV.Kutunza kumbukumbu zote za kikatibu.

5.2.4 KATIBU MSAIDIZI

5.2.4.1 Ni mjumbe wa Kamati ya Fedha na Mikopo.

5.2.4.2 MAJUKUMU YA KATIBU MSAIDIZI
I.Atatekeleza majukumu ya Katibu wakati katibu anapokuwa hayupo kwa udhuru
wowote.
II.Kumsaidia Katibu.
III.Atakaimu nafasi ya Mhasibu endapo Mhasibu hatakuwepo.

5.2.5 MHASIBU
5.2.5.1 Mhasibu atatakiwa kuwa mwenye ajira ya kudumu.
5.2.5.2 Atakuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mikopo.

5.2.5.3 MAJUKUMU YA MHASIBU

I.Kutunza kumbukumbu za fedha za kikundi .
II.Kuandaa na Kutoa taarifa ya Mapato na Matumizi ya nusu mwaka na ya
mwaka mzima.
III.Kuwakumbusha wanakikundi juu ya michango yao na madeni ya kila mwezi.
IV.Kufuatilia mikopo kwa wanachama waliochukua mikopo na kuhakikisha
inarejeshwa kwa wakati.
V. Kutunza vifaa vya kiuhasibu.
VI.Kuandaa vifaa na nyaraka za kiuhasibu.
VII.Ni Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Mikopo.

5.3 KAMATI ZA KIKUNDI

5.3.1 KAMATI YA KATIBA NA SHERIA

5.3.1.1 WAJUMBE WA KAMATI YA KATIBA NA SHERIA

I. Mwenyekiti Msaidizi wa Kikundi (Mwenyekiti wa Kamati).
II. Wajumbe 2 wa kuchaguliwa na kikundi.
5.3.1.2 Mjumbe mmoja wa Kamati hii atakuwa mjumbe wa Kamati ya Fedha na Mikopo.

5.3.1.3 MAJUKUMU YA KAMATI
I.Kusimamia Katiba na Sheria za kikundi.
II.Kuandaa na kutoa fomu za kujiunga na kikundi.
III.Kupendekeza maboresho ya Katiba na Sheria.

5.3.2 KAMATI YA FEDHA NA MIKOPO

5.3.2.1 WAJUMBE WA KAMATI YA FEDHA NA MIKOPO
I. Mhasibu (Mwenyekiti wa Kamati)

KATIBA YA IKICHA
II. Katibu Msaidizi
III.Mjumbe mmoja kutoka Kamati ya Katiba na Sheria.

5.3.2.2 MAJUKUMU YA KAMATI
I.Kusimamia utoaji na urejeshaji wa mikopo.
II.Kuandaa na kutoa fomu za mikopo
III.Kuandaa na Kutoa Taarifa ya Mikopo.
IV.Kutafuta na kufuatilia wapi mikopo inapatikana.
V. Kuandaa na Kutoa taarifa ya Mapato na Matumizi ya nusu mwaka na ya
mwaka mzima.

5.3.3 KAMATI YA MAAFA NA SHEREHE

5.3.3.1 WAJUMBE WA KAMATI YA MAAFA NA SHEREHE

I.Kamati itakuwa na wajumbe watatu (03) wa kuchaguliwa na kikundi.

5.3.3.2 MAJUKUMU YA KAMATI
I. Kutoa Taarifa ya Maafa na Sherehe kwa wanachama.
II. Kupendekeza namna ya kutatua matatizo hayo.
III.Kusimamia michango ya Maafa na Sherehe.
IV. Kuandaa na Kusimamia sherehe za kikundi.

5.3.4 KAMATI YA UCHUMI NA MIPANGO

5.3.4.1 WAJUMBE WA KAMATI YA UCHUMI NA MIPANGO

I.Kamati itakuwa na wajumbe watatu (03) wa kuchaguliwa na kikundi.

5.3.4.2 MAJUKUMU YA KAMATI
I. Kubuni na kuanzisha miradi.
II. Kushauri kikundi masuala ya uchumi.
III.Kuratibu mafunzo ya ujasiriamali kwa kikundi.
IV.Kuandaa malengo ya mwaka.
V Kusimamia miradi ya kikundi.

5.4. MUDA WA UONGOZI
I.Uongozi utakuwa madarakani kwa muda wa mwaka mmoja (1) tu.
II.Kiongozi anaweza kuchaguliwa tena kuwa kiongozi baada ya muda wake wa
uongozi kukamilika.
III. Mwanachama hataweza kuchaguliwa na kuitumikia nafasi moja kwa muda wa
zaidi ya miaka mitatu (03) mfululizo.
IV.Kiongozi aliyetumikia nafasi moja kwa miaka mitatu mfululizo anaweza
kuchaguliwa kwenye nafasi nyingine.

SEHEMU YA SITA
6.0 MIKUTANO NA VIKAO VYA KIKUNDI
6.1 MKUTANO MKUU

KATIBA YA IKICHA
6.1.1 Mkutano mkuu wa kikundi utafanyika mara moja kwa kila mwaka.
6.1.2 Tarehe ya mkutano mkuu kufanyika itapangwa na kikao cha mwezi wa kumi na
mbili (12).

6.1.3 MAJUKUMU YA MKUTANO MKUU
I.Kupokea na kujadili taarifa ya fedha.
II. Kujadili jambo lilojitokeza kama vile kupokea wanachama wapya, kufukuza au
kutoa ushauri kwa wanachama kuhusu mwenendo mzima wa mwanachama.
III.Kujadili mwanachama anayetaka kujitoa.
IV.Kujadili maendeleo ya kikundi ya mwaka.
V.Kupokea na kujadili taarifa za kamati za kikundi.
VI.Kujadili na kupitisha miradi ya kikundi.
VII. Kufanya uchanguzi wa viongozi wa Kikundi.
VIII. Kupanga namna bora ya kuinua kikundi kiuchumi.

6.2 VIKAO VYA KIKUNDI
6.2.1 Kutakuwa na vikao kumi na mbili (12) kwa mwaka.
6.2.2 Vikao vyote kumi na mbili vitafanyika kila Jumapili ya kwanza ya kila mwezi.

6.2.3 MAJUKUMU YA VIKAO
I. Kupokea ADA ya kila mwezi.
II. Kupokea maombi ya mikopo.
III. Kujadili maendeleo ya kikundi.
IV. Kupokea marejesho ya mkopo.
V. Kupokea maombi ya wanachama wapya.
VI. Kujadili ukomo wa mwanachama.
VII. Kupokea mapendekezo ya mabadiliko ya katiba na kanuni.
VIII. Kupokea na kujadili taarifa mbalimbali za kikundi.

6.3 VIKAO VYA DHARURA
I.Kutakuwa na Vikao vya dharura kama ikibidi viwepo.

6.4. KAMATI TENDAJI
6.4.1 Itaundwa na Mwenyekiti,Mwenyekiti Msaidizi,Katibu,Katibu Masidizi na Mhasibu.

6.4.2 VIKAO VYA KAMATI TENDAJI
I Kamati Tendaji itakaa mara moja kwa mwezi kabla ya kila kikao.
II Kamati Tendaji itafanya kikao mwezi mmoja kabla ya Mkutano Mkuu.

6.4.3 MAJUKUMU YA KAMATI TENDAJI
I.Kuandaa agenda za mkutano mkuu.
II.Kuandaa taarifa ya fedha.
III.Kushughulikia masuala ya nidhamu.
IV.Kupitia na kujadili miradi ya kikundi.
V.Kusimamia maendeleo ya kikundi.

KATIBA YA IKICHA
VI.Kujadili maombi ya wanachama wapya.
VII.Kupokea,Kujadili na Kuwasilisha Mapendekezo ya Marekebisho ya Katiba
kwenye Kikao au Mkutano mkuu.
VIII.Kuandaa agenda za Vikao na Mkutano mkuu.
SEHEMU YA SABA

7.0 MAPATO YA KIKUNDI

7.1 VYANZO VYA MAPATO YA KIKUNDI

7.1.1 Ada ya kiingilio
I. Kila mwanachama anapaswa kulipa ada ya kiingilio.
II. Kiingilio ni mali ya kikundi.

7.1.2 Ada ya kila mwezi.
I. Kila mwanachama anapaswa kulipa Ada kila mwezi.

II. Ada ni mali ya mwanachama.
7.1.3 Faida kutokana na Miradi.
7.1.4. Riba ya Mikopo
7.1.5 Faini mbalimbali.
7.1.6 Miradi mbalimbali

7.1.7 MICHANGO MINGINE
I.HARUSI
a) Mwanachama akiwa na Harusi atachangiwa.
II.MAGONJWA
a) Mwanachama akilazwa kuanzia siku tatu mfululizo atachangiwa.
b) Mwanachama atakayepewa rufaa ya matibabu nje ya Wilaya ya Kigoma
atachangiwa .
III.MISIBA
a) Mwanachama akifariki kila mwanakikundi atatoa rambirambi.
b) Mwanachama akifiwa atapewa rambirambi kutoka kwa kila mwanachama.
IV.ANAYEHAMA NJE YA MANISPAA
a) Mwanachama atakayehama nje ya Manispaa atachangiwa.

7.2 MIKOPO
7.2.1 Kila mwanachama atakuwa na haki ya kukopa kwenye kikundi.
7.2.2 MADENI YA KIKUNDI
I.Kila mwanakikundi anahusika kikamilifu na madeni ya kikundi kama si kwa uzembe.
II.Deni binafsi la mwanakikundi si deni la kikundi na kikundi hakitahusika kwa
vyovyote vile.
III.Mkopo utakaohusu kikundi wanachama wote washirikishwe katika hatua zote za
kuchukua mkopo huo na muhtasari uwepo wa kuthibitisha uchukuaji wa mkopo huo.



SEHEMU YA NANE

8.0 UTUNZAJI WA MALI NA FEDHA ZA KIKUNDI
8.1.UTUNZAJI WA MALI NA FEDHA ZA KIKUNDI

I.Kikundi kitakuwa na akaunti benki ambamo fedha zote za kikundi zitatunzwa.
II.Waweka sahihi katika akaunti watakuwa ni :-
a) Mwenyekiti wa Kikundi.
b) Mhasibu wa Kikundi.
c) Katibu wa Kikundi.
d) Mwanachama mmoja ambaye si mjumbe wa Kamati Tendaji.
8.2.UPOTEVU NA UHARIBIFU WA MALI YA KIKUNDI
I. Iwapo itabainika mwanakikundi amepoteza au kuharibu mali ya kikundi itabidi
alipe au afidie upotevu huo au uharibifu huo .Endapo atashindwa kutekeleza agizo
alilopewa sheria na taratibu za kikundi na za nchi zitafuatwa.

SEHEMU YA TISA

9.0 MAREKEBISHO YA KATIBA NA KUVUNJIKA KWA KIKUNDI

9.1 MAREKEBISHO YA KATIBA YA KIKUNDI

I.Marekebisho ya Katiba yatafanyika endapo kutakuwa na uhitaji.
II.Marekebisho ya Katiba yatafanyika iwapo robo tatu ya wanachama wameridhia.
III.Mapendekezo ya Marekebisho ya Katiba yatawasilishwa kwenye kamati ya Katiba
na Sheria kwa maandishi.

9.2 KUVUNJIKA KWA KIKUNDI
I. Kikundi kitavunjika iwapo robo tatu ya wanachama wameridhia.
II.Kufutiwa usajili na Serikali.

SEHEMU YA KUMI


10.0 ORODHA YA WANACHAMA

NA      MAJINA KAMILI                         JINSIA                          WADHIFA                    
1 ELIAS LUZARIA                                     ME                                  MJUMBE                      
2 MAKOKO OBADIA                                ME                                   MJUMBE                      
3 KELVIN E. NGOWI                                 ME                                   MHASIBU                    
4 FILBERT S.LUKONDO                           ME                                    MJUMBE                    
5 KULWA MATHIAS                                   ME                                   MJUMBE                     
6 VITUS TONDELO                                     ME                                   MJUMBE                     
7 SCOLA WILSON                                        KE                                   KATIBU                    
8 EMMANUEL MSABAHA                         ME                                  MJUMBE                      
9 LEAH MOSES                                             KE                                 MJUMBE                     
10 ALEX KAMALINGE                                 ME                               MWENYEKITI                  
11 VERONICA MGOZI                                 KE                                 MJUMBE                   
12 ABDALLAH JUMA                                   ME                               MJUMBE 
13 NEEMA TITO                                            KE                                MJUMBE
14 ZUBERI MROGORO                              ME                                  MJUMBE
15 MARUZUKU SELEMANI                       ME                                MJUMBE
16 NICHOLOUS NDELE                             ME                                  MJUMBE
17 SAMWEL JOSEPH                                  ME                                  MJUMBE
18
19

No comments:

Post a Comment